• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Municipal Council
Lindi Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mazingira na Usafi
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
    • Mtandao wa Barabara
    • Maliasili
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipangomiji na Maliasili
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba za vikao
    • Ratiba ya kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Picha
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
  • E-Learning
    • Joining instructions form
    • past papers
    • Notes

MANISPAA YA LINDI YAZINDUA JENGO LA MAMALISHE SABASABA.

Imetumwa: November 6th, 2020

Katika kuendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kila halmashauri kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato yake ya ndani, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imeviwezesha kiuchumi vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Katika mwaka 2019/2020, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ilitenga Tshs 102,793,499.97 kwa ajili ya kuvikopesha vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu.Aidha ,ilitenga Tshs 59,293,500.00 kwa ajili ya kukopesha kikundi cha Mamalishe Sabasaba, pesa ambazo ndizo zilizotumika kujenga jengo la Mamalishe Sabasaba Manispaa ya Lindi kama linavyoonekana kwenye picha hapo chini:


Katika mwaka wa fedha 2020/2021, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imetenga Tshs 208,224,000.00 kwa ajili ya kuvikopesha vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu. Aidha, hadi kufikia 31 Oktoba, 2020 jumla ya Tshs 83,292,500.00 zilikuwa zimeshakopeshwa kwa vikundi 14 vikiwemo vitano (5) vya Wanawake, sita (6) vya Vijana na vitatu (3) vya watu wenye ulemavu.

Kikundi cha Mamalishe Sabasaba kinaundwa na Wanawake kumi na nne (14) ambao wote ni Mamalishe.Kikundi hiki kimetambuliwa na Halmashauri na kupewa cheti cha utambuzi chenye Na.LMC/CBO/946. Mara baada ya kuomba mkopo kutoka Halmashauri na kupatiwa pesa hizo, wamezitumia kujenga jengo lenye jumla ya vyumba kumi (10), kuweka milango na madirisha ya vyuma (Grill), kutengeneza mfumo wa maji taka pamoja na mfumo wa umeme na kununua samani (viti 60 na meza 10) vyote vya plastiki. Aidha, wameshailipa TANESCO gharama zote za kuingiza umeme katika jengo hilo.

Lengo la kikundi cha Mamalishe Sabasaba kuchagua kujenga jengo hilo ni kuboresha mazingira ya kufanyia shughuli zao za kupika na kuuza vyakula.Hii itapekelekea wananchi wengi na wa aina zote kuhamasika kupata huduma mahali hapa na hatimaye kuwawezesha kujiongezea mapato yao yatakayosaidia kuinua hali za maisha katika kaya zao.

Baada ya uzinduzi wa jengo hilo, Katibu tawala wa Wilaya ya Lindi ndugu Thomas Safari na kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi ndugu Baptista Kihanza waliwaasa Mamalishe wote watakaopata fursa ya kupata vyumba katika jengo hilo kuwa waangalifu katika matumizi ya jengo hilo na kulitunza ili vizazi vijavyo viweze kulitumia pia. Aidha Mamalishe walishukuru sana kwa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kwa kuwapatia fursa hiyo ambayo ni adhimu kwao na kuahidi kulitunza jengo hilo.

Baadhi ya Mamalishe wakiwa na nyuso za furaha katika uzinduzi wa Jengo la Mamalishe Manispaa ya Lindi.


Muonekano wa ndani wa moja ya chumba cha jengo la Mamalishe Manispaa ya Lindi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KATIKA MRADI WA MAJI RUTAMBA. January 07, 2021
  • FURSA ZA UWEKEZAJI MANISPAA YA LINDI June 10, 2020
  • FOMU YA MAOMBI YA KUNUNUA KIWANJA June 25, 2020
  • Semina ya uchaguzi kwa walioteuliwa kuwa wasimamizi wa vituo, wasimamizi wasaidizi na karani waongozaji October 15, 2020
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI NA CHA NNE.

    January 15, 2021
  • MKUU WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI MEJA JENERALI IM MHONA ATEMBELEA MANISPAA YA LINDI

    January 13, 2021
  • MKURUGENZI AAHIDI KUFANYA UKARABATI MASHULENI

    January 06, 2021
  • KITUO CHA AFYA MNAZIMMOJA KIMEANZA KUTOA HUDUMA YA UPASUAJI.

    January 05, 2021
  • Ona Yote

Video

Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi, Jomaary Satura azungumzia ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba 2019.
Video Zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Zabuni
  • sheria mbalimbali
  • Ratiba za vikao
  • Orodha ya Madiwani
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Historia ya Manispaa ya Lindi
  • Miradi inayoendelea
  • Mfumo wa Vibali vya Safari Nje ya Nchi

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • OR - TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Municipal Director

    Anuani ya Posta: 1070 Lindi

    Simu: +255232202164

    Simu ya mkononi: +255767042958

    Barua Pepe: info@lindimc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Vigezo na Masharti
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2020 Manispaa ya Lindi. Haki zote zimehifadhiwa